
Babutale, Madam Rita na Kayumba
“Katika harakati za kutafuta majibu ya kwa nini washindi wa BSS hawafanyi vizuri kwanza nitakujibu kama mdau wa muziki, pili kama mshiriki wa EBSS 2012 pekee kutoka Mwanza aliyetolewa katika Top 09,” anasema.
“Kwanza tatizo kubwa la BSS ni kutopromote ubunifu. Haiwajengi washiriki wake katika kujitegemea kwenye utunzi na uimbaji. Shindano limebase kwenye kuimba covers, na hapa naenda mbali zaidi cover zinatakiwa ziimbwe kama original songs, no improvision sababu ukifanya hivyo utaonekana haujautendea haki wimbo.”
Ameendelea, “Pili, washiriki na hata ma judge wanawaza sana kuhusu ile million 50 itaenda kwa nani kuliko kuwaza katika ni mshiriki gani atakuwa brand mpya ya music na anaweza kusimama na kuuteka umma kwa performance, hili hupelekea kutumia kigezo kimoja tu kumpa mtu ushindi.

Majaji wa BSS, Madam Rita na Master J
“Nne ni elimu,” anaendelea. “Ni ukweli mchungu ila tuumeze tu ili tujifunze. Washiriki wengi wa BSS ni vijana wadogo sana kiumri na kielimu pia. Na wengi wao hutoka katika familia zenye kipato kidogo. Kwa hiyo wanapoingia mle kwenye shindano kwanza wanaona kama bahati. Pili nafasi pekee ya kijikwamua, tatu wanakuwa hawatambui haki zao na kubwa zaidi wanakuwa hawajajiandaa kuupokea u star. Ndio maana wengi wao kama sio wote hawawezi kusimama peke yao mara baada ya mashindano. Na wengine wakishaupata u star, kutokana na kukosa elimu ya kutosha kunawafanya wanakuwa malimbukeni hivyo kuishia kuharibu vipaji vyao.”
“La mwisho, Judges wajenge a fair platform kwa washiriki wote ili kupata washindi wa kweli, mihemko ipungue, wasitake sides, na wasiwe na personal interest kwa washiriki ili kupata mshindi wa kweli. Amini nakwambia katika most of the time, the best singers never win competition. Kwa kusema hilo pengine waimbaji bora hutolewa kwa vigezo(vya kijinga) vingine tu ili majaji waonekane wana power lakini matokeo yake ndio haya tunayoyaona. Their winners never move even a baby step ahead. Ni matumaini yangu umejifunza kitu.”
0 maoni: