Muimbaji huyo Alhamisi hii aliialika Bongo5 kuitembelea studio hiyo
mpya iliyopo Sinza Palestina jijini Dar es salaam ili kujionea uwekezaji
aliofanyika.
Bella ameiambia Bongo5 kuwa studio hiyo itamfanya afanye kazi zake kwa utulivu zaidi tofauti na awali.
“Lengo la kwanza la kuanzisha hii studio nilikuwa nataka nipate muda
wakutosha wakufanya kazi zangu, kwamba hata saa sita usiku nikipata idea
ninafungua studio nafanya kazi,” alisema Bella “Sio mpaka uanze
kumtafuta producer ambaye anakupa promise ya wiki ijayo mpaka filling
zinaondoka. Lakini sasa hivi nikipata filling hata saa nane usiku
naingia studio nafanya kazi kwa sababu ipo kwajili yangu,”
Aliongeza, “Cha pili ni kusaidia vipaji pamoja na biashara, kwa
wanaotaka kuja kurekodi mimi nawakaribisha tena nitakuwa natoa mchango
hata wamawazo hata nikitakiwa kufanya nao kolabo nitaangalia mtu ambaye
anafaa nitafanya naye,”
Pia muimbaji huyo amesema kukamilika kwa studio kunamfanya aanze mara
moja mchakato wa kuandaa albamu yake mpya ambayo itakuwa na kolabo za
mastaa wa nje.
0 maoni: